Pigo Kwa Manchester United

Mchezaji wa Manchester united Alexis Sanchez anahofiwa kuwa nje kwa mwezi miwili kwa kupata majeraha.
 
Mchile huyo alipata majeraha kwa magoti kwenye mechi yao dhidi ya Southhampton siku ya Jumamosi na kulazimishwa kutoka nje baada ya dakika 52 tu za mchezo.

Daktari wa timu ya Chile,Pedro Onate amesema Sanchez anapaswa kuwa nje kwa takriban mechi nane ili kutibiwa na kupona vikamilifu

Sanchez atakosa mechi ya marudiano dhidi ya PSG kwenye kombe la kung'ang'ania bingwa la taji ya Europa EUFA  kabla kukosa dhidi ya Arsenal na Wolves .

Mchezaji huyo wa kati ameianzia Manchester united kwenye kumi na moja bora mara nane huko akifunga bao moja.

Sanchez mwenye umri wa  miaka 30 amekuwa na wakati ngumu tangu kuungana na Manchester United mwezi wa Januari mwaka jana.

Alexis amefunga mabao tano tu kwa mechi 40 alizochezea Manchester.


Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals