Mahakamani
Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeairisha
kesi inayomkabili Geofrey Odhiambo anayeshtakiwa kwa kosa la kuiba .
Vilevile
Mbele
ya hakimu Fatuma Rashid, mahakama
iliambiwa kuwa mwanamme huyo pamoja na wengine ambao hawakufiki mbele ya
mahakama walimwibia Philip Nyamonga miti za uzio kwa boma pamoja na
rolls kumi za nyaya mnamo tarehe 9 disemba mwaka 2018 kwenye eneo la
Wath Orengo iliyo kisumu east,kisumu kaunti.
Bidhaa zote ni za gharama ya thamani elfu 70000
Geofrey alikanusha mashtaka hayo, na kuomba
kuachiliwa huru.
Aliachiliwa na kuagizwa kuleta mashaidi wake siku ya kesi hiyo kusikilizwa.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 23 mwezi Mei,
mwaka huu. Vilevile
Mwanamme mmoja kwa jina Peter Omondi ameshtakiwa kwenye hiyo ya Winam jijini Kisumu kwa kosa la kukiuka sheria za barabara.
Mbele
ya hakimu Fatuma Rashid, mahakama iliambiwa kuwa mshtakiwa alipatikana
mnamo tarehe 18 mwezi huu kwenye barabara ya kisumu kakamega akiendesha
gari bila leseni,bila sare ya dereva na pia kuendesha gari lisilofaa kwa
barabara.
mshtakiwa alikanusha mashtaka na kuomba kuachiliwa kwa dhamana.
Aliachiliwa kwa dhamana ya shillingi alfu thelathini.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 6 mwezi Juni, mwaka huu.
Comments
Post a Comment