Ombi la Kogalo lakataliwa!

Shirikisho la soka nchini KPL imekataa ombi la Gor mahia ya kuairisha mechi yao dhidi ya kakamega homboyz inayopaswa kuchezwa siku ya alhamisi.
Kogalo wameomba kutoshirikishwa kwenye mechi hiyo ya ligi ili kuwapa muda wa kutosha ya kujitayarisha kwa mechi yao ya mwisho kwenye kikundi cha D  kwenye kombe la Caf Confederation.
Gor mahia walipoteza dhidi ya Zamalek nchini Egypt kwa mabao nne kwa sufuri hivyo basi ni lazima washinde mechi yao ya mwisho dhidi ya Petro Atletico siku ya jumapili.
Kocha wa Gor mahia Hassan Oktay amesema kuwa wachezaji wake wanahitaji kuenda kwenye mechi hiyo wakiwa asilimia 100 ili kuhakikisha wameshinda na kujipea nafasi kwenye robo fainali.

Afisa mkuu mtendaji wa KPL Jack Oguda amekataa ombi hilo na kusema kogalo wako na zaidi ya saa 72 ya kujiandaa baada ya mechi yao ya Alhamisi.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals