Mahakamani

Mwanamme mmoja kwa jina Brian Opiyo Okumu, ameshtakiwa kwenye mahakama ya Winam jijini Kisumu kwa kosa la kuiba ng'ombe.
Mbele ya hakimu Jackline Mitei, mahakama iliambiwa kuwa mshtakiwa alimwibia Richard Ajango ng'ombe mwenye dhamana ya shilling alfu 45 mnamo tarehe 4 mwezi huu, eneo ya Koluwa kaunti ya kisumu .
Mshtakiwa alikanusha mashtaka, na kuomba kuachiliwa dhamana.
Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 25 pesa taslimu, au shilingi alfu 50 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 4 mwezi Juni, mwaka huu

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals