KOGALO WAIBIWA!!!

Timu ya Gor mahia amaarufu kama Kogalo pamoja na mashabiki wanalalamika kuibiwa bao siku ya jumapili walipokuwa wanacheza kwenye mkondo wa pili dhidi ya NA Hussein Dey kwenye kikundi chao kwa mechi za  kung'ang'ania bingwa barani Africa CAF.

Kogalo wanasema walinyang'anywa bao mnamo dakika ya 59 baada ya defenda Shafiq Butambuze kufunga kwa kichwa chake kutoka kwa krosi iliyopigwa na Francis Kahata.

Mwamuzi wa mechi hiyo kutoka mali aliamua kuwa mlinda lango wa Hussein Dey alichezewa visivyo iilhali pich za video zinaonyesha kweli kuwa mlinda langu huyo alijingoga na mchezaji wake mwenyewe huko wakijaribu kuondosha hatari.

Uamuzi huo ulilazimisha kogalo kurudi nyumbani bila pointi.

Gor mahia wamesukumwa hadi nafasi ya pili na pointi sita baada ya kushindwa hivyo ni lazima wajitahidi kushinda ugenini dhidi ya Zamalek ya Egypt kabla ya kuaiandaa Petro Atletico mnamo tarehe 17 mechi.

Gor mahia wanaitaji kumaliza miongoni mwa timu mbili bora katika kundi hilo la D ili kujipa tiketi kwenye robo fainali.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals