Mahakamani
wanaume wawili kwa majina Francis Otieno Ogello na Elijah Okumu Owiti, wameshtakiwa kwenye mahakama ya Winam jijini
Kisumu kwa kosa la kumpiga mwanada Valary Barasa .
Mbele
ya
hakimu Jackline Mitei, mahakama iliambiwa kuwa washtakiwa pamoja na
wengine ambao hawakufika kotini walimpiga na kumuumiza Valary mnamo
tarehe20 mwezi February mwaka huu kwenye eneo la chemelil kaunti ya
kisumu.
washtakiwa
walikanusha mashtaka.
Kesi hiyo
itatajwa tarehe moja mwezi wa nne, mwaka huu.
Kesi zingine zilizokuwa mbele ya mahakama ni pamoja na;
Kesi inayomkabili Erick Nyamongo Nyamache anayetuhumiwa kuibia Charles Otieno Oluoch bidhaa za thamani ya alfu 13 mnamo tarehe 6 mwezi wa saba mwaka jana mtaani Nyamasaria.
Kesi inayomkabili Eliakim Mwalu anayetuhumiwa kumwibia Faith Kalacia simu aina ya samsung yenye thamani ya alfu kumi na tatu na mia tano mnamo tarehe 28 mwezi february mtaani Mamboleo jijini Kisumu.
Kesi inayomkabili David Oruko Otieno anayetuhumiwa kumpiga na kumuumiza Christine Adhiambo mnamo tarehe nne january mwakani kwenye eneo la Rapogi iliyoko kaunti ya kisumu.
Kesi inayomkabili Peter Oduor Owiti anayetuhumiwa kumnajisi msichana mwenye umri wa miaka kumi na mbili mnamo tarehe 13 mwezi huu.
Comments
Post a Comment