Mwanamme mmoja kwa jina Erick Omondi ameshtakiwa kwenye mahakama ya Winam jijini Kisumu kwa tuhuma ya wizi.
Mbele ya hakimu Jackline Mitei, mahakama iliambiwa kuwa mshtakiwa pamoja na wengine ambao hawakufika kotini walivunja maktaba na kuiba vitabu pamoja na vitu vingine enye thamani ya shillingi alfu 48200 mnamo tarehe 13 mwezi wa Agosti mwaka jana kwenye shule ya sekondari ya wasichana st.Ignatious Loyola iliyoko manyatta kaunti ya kisumu.
mshtakiwa alikanusha  mashtaka.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 26 mwezi Aprili, mwaka huu.
Vilevile,mahakama hiyo imetupilia mbali kesi inayomkabili Philip Nyadero anayetuhumiwa kuibia kampuni ya Kinagor dairy vitu vya thamani ya shilingi alfu 140000.

Mbele ya hakimu Jackline Mitei, Mahakama iliambiwa kuwa baada ya kuchunguza vizuri kampuni ya kinagor imepata kwamba bwana Philip hana hatia kwa hivyo waliomba mahakama kumwachilia.


Bwana Philip Nyadero aliachiliwa huru.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals