Ligi Kuu Nchini
Mechi kadhaa za ligi kuu ya soka nchini-kpl,zimechezwa hivi leo kwenye uga tofauti kote nchini.
Mabingwa
wa ligi mara kumi na saba Gor mahia almaarufu kogalo wameilaza Zoo
Kericho kwa mabao manne kwa sufuri kwenye mechi iliyoandaliwa ugani
Green stadium Kericho.
Nahodha Denis Oliech alicheka na wavu
mara mbili mtawalia kabla ya Kenneth Mugana na Nicolas kipkirui
kujiandikisha katika kitabu cha wafunga bao.
Matokeo mengine ni kama yafuatayo;
Timu ya sofapaka imeshinda mt.Kenya kwa mabao tatu kwa moja ugani Kenyatta.
Kakamega homeboyz wamepiga Bandari fc kwa mabao mawili kwa moja ugani Mbarika sports club.
Tusker fc wameshinda Kariobangi Sharks kwa mabao tatu kwa moja ugani ruaraka.
Huko Ulinzi stars wakiilaza Sony sugar kwa mabao mawili kwa moja ugani Afraha.
Vihiga united wametoka sare ya mabao mawili kwa mawili dhidi ya FC leopards ugani Bhukungu.
KCB wakitesa nyasi bure dhidi ya Western Stima na kutoka na sare ya bao moja kwa moja ugani Nairobi City Stadium.
Comments
Post a Comment