Yaliyotekea Kwenye Ligi Kuu Uingereza
Timu ya Chelsea wameongeza matumaini yao ya kumaliza ligi ligi kuu ya Uingereza kwenye nne bora,hii ni baada ya kutoka nyuma bao moja na kushinda Cardif City kwa mabao mawili kwa moja siku ya jumapili ugani Cardif. Cardif City walipata bao mnamo dakika ya 46 mguu yake Víctor Camarasa lakini Chelsea walijibu bao hiyo kipindi cha pili mnamo dakika ya 84 kupitia kwa nahodha yao Cezar Azpilicueta kabla ya Rouben Loftus Cheek kuingizwa dakika za ushee na kufunga bao la ushindi kutoka kwa krosi yake Wilian. Mchezaji bingwa raia wa Ubelgiji Eden Hazard alileta matumaini kwa timu ya Chelsea alipoingizwa baada ya timu hiyo kushindwa kupata bao. Ushindi huo imempea Meneja Maurizio Sarri afueni baada ya mashabiki kutaka afutwe kazi . Matokea hiyo pia ina maana kuwa chelsea wako kwenye nafasi ya tano wakitoshana na Arsenal na pointi 60,huko wakiwa pointi moja nyuma ya Manchester United. Meneja wa Cardif Warnock hakufuraishwa na maamuzi ya bao la Azpilicueta huko a...