Waaguzi watisha kugoma
Kuna hofu baina ya wakazi wa kisumu hasa jamaa na
marafiki za wagonjwa katika mahospitali mbalimbali za uma.Hii wasiwasi
inakuja baada ya shirikisho linalosimamia waaguzi kuonya kuwa wataenda
mgomo mnamo Juma tatu tarehe nne mwezi huu.Waaguzi hao wanadai kuwa
serikali haijatimiza makubaliano yao ya kuwapa marupurupu mbalimbali na
kupandishwa cheo kutokana na maelewano kati yao mnamo November 2011.
Tulipozungumza
na mkurugenzi mkuu wa Afya wa Kisumu county bwana Stephene Otieno Sewe
alisema bado wanafanya juhudi zote kuhakikisha kwamba matakwa ya waaguzi
hao yametatuliwa.
Tukisalia kwa habari za afya,wakazi wa
kisumu bado wanajitokeza kwa sehemu tofauti ya kaunti ili kusajiliwa na
uhc.Kumbuka shughuli hiyo ya kusajili watu ilifaa kukamilisha jana
tarehe 31 lakini imesukumwa mbele hadi tarehe 23 mwezi huu ili kupatia
muda wale ambao hawajajisajili kuja kujiandikisha .
Mkurugenzi mkuu wa afya,kisumu kaunti Bwana Stephene Otieno Sewe
ameimiza wakazi wa kisumu kujitokeza kijiandikisha na huduma ya afya ya
kupatiana matibabu ya bure almaarufu kama UHC.Amesema kwa sasa hivi watu
takriban 650,000 tayari wamejiandikisha na uhc hivyo basi inabakisha
watu karibu 550,000 ambao hawajajisajili,kumbuka kisumu kaunti iko na
watu takriban milioni moja nukta mbili.
Vilevile bwana Sewe
amesema kwamba wameheka mikakati mbalimbali,zikiwa pamoja na kutuma
ajenti kwa shuleni mbalimbali ili kupata takwimu yao ikilanganishwa na
ya wazazi,kutuma ajenti kwa hospitali mbalimbali na pia kuna wale watu
wa afya wanaojitolea kutoka kwa jamii kuhakikisha kwamba hakuna
mwananchi anakosa kusajiliwa na uhc.
Comments
Post a Comment