Timu ya Atletico Madrid ilicharaza vijana wa Juventus kwa mabao
mawili kwa sufuri kwenye mkondo wa kwanza za mechi za raundi ya kumi na
sita ya kombe la Eufa.Mechi hiyo ilichezwa usiku wa jumanne kwenye
uwanja wa Wanda Metropolitano nyumbani kwa Atletico madrid.
Atletico
walipata bao lao la kwanza kupitia kwa defender wao Jose Gimenez mnamo
dakika ya 78 kabla ya Diego Godin kuongeza la pili dakika tano baadaye.
Juhudi zake mchezaji
bingwa Christiano Ronaldo kupatia timu yake ushindi iligonga mwamba na
hata za mwenzake mpotugali Diblo Dyballa pia hayakufua dafu uko wakishindwa na
Vijana wa Diego Simeon.
Kwingineko,Vijana wa Pep Guardiola
Manchester City walishinda Schalke 04 kwa mabao matatu kwa mawili
ugenini Veltins Arena kwa wanaSchalke04.
Manchester city
ndiye waliotangulia kufunga mnamo dakika ya 18 kupitia kwa mchezaji
Sergio Kun Aguero lakini wanaSchalke 04 walijibu kwa mpigo kwa mabao
mawili mnamo dakika ya 38 na 45 mtawaliwa,bao zote za schalke zilifungwa
kupitia kwa kituta cha penalti na mchezaji Nabil Bentaleb baada ya
wanamancity kucheza visivyo.
Mambo yalianza kuenda segemnenge
kwa vijana wa pep baada ya Nicolas Otamendi kuonyeshwa kadi nyekundu
mnamo dakika ya 68 lakini walipata nafuu dakika ya 85 ambapo Lorey sane
alifunga bao la pili na kusawazisha mambo kabla ya Raheem Sterling
kufunga bao la ushindi dakika ya 90.
Comments
Post a Comment