mwanaume ashtakiwa mahakamani na kosa la kunajisi msichana
Mwanaume mmoja anayefahamika kama Erick Odhiambo amefikishwa mbele ya mahakama ya Winam jijini Kisumu .Erick anatuhumiwa kumnajisi msichana mwenye umri wa miaka kumi na saba.
Mbele
ya hakimu Fatuma Mwanza Rashid, mahakama
iliambiwa kua bwana Erick alifanya kitendo hicho mnamo tarehe 20 mwezi
huu wa February kwenye mtaa wa mamboleo iliyoko
kisumu.
Erick alikanusha mashtaka hayo, na kuomba
kuachiliwa dhamana.
Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 125 pesa taslimu, au shilingi alfu 250 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 9 mwezi Mei,
mwaka huu.
Comments
Post a Comment