mchezoni

Ligi kuu nchini KPL itarejea leo kwa mechi moja ambapo Gor Mahia almaarufu kama Kogalo wataandaa vijana wa western stima kwenye uga wa Moi International Sports Centre,Kasarani.Mechi hiyo itachezwa saa kumi alasiri.Kumbuka Kogalo wako nafasi ya tatu kwenye jedwali ya ligi wakiwa na alama 25 baada ya kucheza mechi 12{mechi moja nyuma ya viongozi Bandari ambao wako na alama 28},Western Stima nao wako nafasi ya 7 na alama 20.
Kwingineko mechi za kombe la Eufa ziliendelea usiku wa juma nne kwa mechi mbili tofauti.Barcelona walilazimishwa kutoka sare bila bao lolote ugenini kwa Olympique Lyonnais,juhudi zake mchezaji bingwa Lionel Messi kupatia timu yake bao iligonga mwamba na kuwalazimisha kugawa alama.
Liverpool pia walitesa nyasi bure ugani Anfield walipoandaa Bayern Munchen.
Mechi zingine zitaendelea leo usiku ambapo Atletico Madrid wataandaa Juventus,vilevile Fc Schalke 04 watakaribisha vijana wa Manchester city.Mechi zote zitachezwa kuanzia saa tano.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals