Mahakamani
Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeahirisha
kesi inayomkabili Collince Otieno Ogello anayetuhumiwa kupokea pesa kwa njia za udanganyifu.
Mbele
ya hakimu Joseline Mutehi, mahakama
iliambiwa kua mwanamme huyo alipokea pesa kutoka kwa Benard Oyalla,
akidai kua yeye ni ajenti wa Eldama comfort house iliyoko mtaani Bandani
jijini Kisumu.
Benard amesema kuwa alimpa Collince shilingi 10,000
akiahidi kuwapa huduma za Eldama comfort house.
Collince Otieno alikanusha mashtaka hayo, na kuomba
kuachiliwa dhamana.
Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 5 pesa taslimu.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 9 mwezi April,
mwaka huu.
Comments
Post a Comment