Mwanamme mmoja kwa jina Baraka Churchil Otieno , ameshtakiwa kwenye mahakama ya Winam jijini Kisumu kwa kumnajisi msichana mwenye umri wa miaka 11.
Mbele ya hakimu Benard Kasavuli, mahakama iliambiwa kua mshtakiwa alitekeleza uhalifu huo tarehe 19 mwezi huu, mtaani Obwola  jijini kisumu.
Mshtakiwa alikanusha mashtaka, na kuomba kuachiliwa dhamana.
Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 100 pesa taslimu, au shilingi alfu 200 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe  11 mwezi Machi, mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals