Mahakamani:wanawake taabani
Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeahirisha
kesi inayomkabili Fiona Awino anayetuhumiwa kuumwibia mwajiri wake kwa jina la purity Anyango .
Mbele
ya hakimu Fatuma Mwanza Rashid, mahakama
iliambiwa kua mwanadada huyo alimwibia mdozi wake pesa takriban elfu
hamsini na nane na mia sita mnamo juma mosi tarehe kumi na sita mwakani
uko mtaa wa car wash iliyoko kisumu.
Fiona alikanusha mashtaka hayo, na kuomba
kuachiliwa dhamana.
Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 50
pesa taslimu, au shilingi laki moja na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 8 mwezi Aprili,
mwaka huu.
Tukisalia
mahakamani,Samantha Atieno alikubali mashtaka baada ya kuhutumiwa kuuza
pombe bila leseni kwenye mtaa wa molem ilioko jijini kisumu.Alitozwa
faini ya alfu ishirini ama mwezi sita gerezani.
Comments
Post a Comment