Mchuano za KPL
Mechi za kung'ang'ania kombe la KPL zitaendelea wikendi hii kwenye
uga tofauti nchini.Kumbuka Mathare united ndiye bado wanaongoza kwenye
jedwali ya kombe hilo.
Mechi izo zitang'oa nanga kesho mnamo
saa nane mchana na mchuano kati ya Mount Kenya United Fc na Viongozi wa
jedwali Mathare united kwenye uga wa Nyayo jijini nairobi.Kisha posta
rangers watajibwaga ugani kipchoge keino stadium kuchuana na Tusker fc
mnamo saa tisa jioni.Vilevile Ulinzi stars watacheza na chemelil ugan
Afraha iliyoko nakuru mnamo saa kumi na robo.
Mech
zingine zote zitaendelea siku ya jumapili saa tisa jioni zikiwemo
Kakamega homeboyz dhidi ya Vihiga united kwenye uga wa Afrah.Nzoia sugar
pia watacheza dhidi ya Sony Sugar kwenye uga wa Masinde Muliro iliyoko
Bungoma .
Vilevile Mabingwa wa kombe la sportpesa kariobangi
Sharks pia wataendeleza kampeni zao dhidi ya sofapaka fc ugani Nairobi
city stadium.Vijana wa Zoo kericho pia watamenyana na Kenya Commercial
Bank ugani Green stadium Kericho.
Kisha Bandari fc watamaliza shughuli izo kwa kualika Fc Leopards kwenye uga wa Mombasa stadium .
Comments
Post a Comment