Kogalo watishwa

Kocha ya timu ya Hussein Dey kutoka Algeria ametisha kuonyesha Gor mahia madharau walionyeshwa Nairobi kabla ya mechi yao siku ya juma pili waliopoteza kwa mabao mawili kwa sufuri. 
Kocha huyo anadai kuwa hawakupewa basi na hata walifanya mazoezi kwenye uga ya kucheza kriketi kisha wakatupiwa vitu kwa uwanja walipokuwa wakichuana.  
Kocha huyo ameahidi wanakogalo kuwa pia wao watafanyiwa vivyo hivyo wanapoenda ugenini kule Algeria wikendi. 
Amepeleka malalamishi kwa tume ya kusimamia mpira Africa CAF na pia wasimamizi wa mechi hiyo.
Kogalo nao wamesema hawaogopi chochote wanapojiandaa kumenyaana siku ya juma mosi kule Algerias na liwe liwalo.
 

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals