Sarri taabani
Timu ya Chelsea hawakutuzwa kwao Stamford Bridge walipolazwa mabao
mawili kwa sufuri na timu ya Manchester United kwenye mechi ya raundi ya
tano ya kipute cha FA jana usiku.Hivyo basi chelsea wamebanduliwa
kutoka kwa mashindano hayo.
Matokeo hayo yanauweka uongozi wa
mkufunzi wa Chelsea Sarri katika hali mbaya,huko united ikijibu baada ya
kushindwa kwa mara ya kwanza chini ya ukufunzi wa Ole Gunna Soljkskjear
na kujinyakulia nafasi kwenye robo fainali dhidi ya Wolvehampton.
Ander
Herrera alifunga bao la kwanza baada ya kupata krosi nzuri kutoka kwa
Paul Pogba mnamo dakika ya 31 kabla ya Pogba kuongeza bao la pili
kupitia kichwa dakika chache kabla ya mapumzikoni.
Tukisalia mchezoni,Liverpool itaiandaa Bayern Munchen kwenye mechi ya kikundi cha Eufa leo usiku.
Mechi hiyo itachezwa ugani Anfield kuanzia saa tano za usiku.
Vilevile Timu ya Barceleona itakuwa ugenini dhidi ya Olympique Lyonnais kwenye kampenzi za kombe hilo la Eufa,
Comments
Post a Comment