spoti

Timu ya Gor mahia Almaarufu kama Kogalo leo hii itamenyana na timu ya Tusker fc mnamo saa kumi alasiri ugani Kasarani.
Kogalo wapo kwenye nafasi ya tatu na pointi 26 kwenye jedwali ya ligi kuu ya kenya KPL baada ya kucheza mechi 13 uko wapinzani wao Tusker wakishikilia nafasi ya sita na pointi 22.
Tukisalia mchezoni,mechi mbalimbali za EPL zitarejea leo usiku ili kuendeleza kampeni za kushinda kombe hilo,
Mechi hizo zitaanza mida ya saa nne kaso robo ambapo,
Arsenal almaarufu kama the gunners watawalika vijana wa Bournemouth ugani emirates.
Southampton wataiandaa Fulham fc ugani s.t Marys kabla ya mabingwa watetezi Manchester City kujibwaga ugani Etihad dhidi ya westham united mida ya saa tano kamili.
Chelsea watacheza kwao Stamford Bridge dhidi Totenham Hotspurs uko Liverpool wakiandaa Watford ugani Anfield.
Manchester Unted almaarufu kama mashetani nyekundu watecheza ugenini Selhust Park dhidi ya Crystal Palace.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals