Posts

Showing posts from February, 2019

Jumbe za rambirambi kwa mwana-mziki Kantai

Image
 Wakenya mbalimbali wanazidi kutuma ujumbe za rambi rambi kwa jamaa,marafiki na familia ya Marehemu mwana-mziki Chris Kantai. Kantai alifariki siku ya jumatano asubuhi kwenye hospitali ya St.Francis jijini Nairobi ambapo amekuwa akilazwa kuanzia jumatatu baada ya kuanza kuuguwa. Kupitia ujumbe kutoka kwa mwakilishi wa familia Wanjiku Thuku,amesema kwamba Chis Kantai ambaye anayefaamika sana kwa nyimbo zake zilizovuma kama Huu Ni Nani,Ting' Badi Malo akimshirikisha Khaligraph Jones  na hata Happy wakiimba na mwanadada STL,alikufa baada ya kuwa na shida ya kupumua. Ameongeza kwamba mipango za kuandaa mazishi zinaenedelea na atazidi kueleza mashabiki na marafiki siku ya kumzika mwenda zake Chris. Kantai ameecha nyuma bibi na mtoto mmoja.Atakumbukwa kwa nyimbo zake mbalimbali zilizovuma na pia  itakumbukwa kuwa Kantai ndiye aliyeleta mwana-mziki bingwa Stella mwangi kwenye miziki na ngoma yao ya Happy. Amefariki akiwa na umri wa miaka 42. Wanamziki mbalimbali wametoa ...

Sarri Apata Afueni Baada Ya Ushindi Ya Chelsea Dhidi Ya Totenham

Image
Mkufunzi wa timu ya Chelsea Maurizio Sarri amepata afueni na matumaini ya kubakia kama meneja wa chelsea baada ya ushindi wao dhidi ya Totenham kwenye mechi ya kung'ang'ania taji la ligi kuu Uingereza-EPL.  Sarri alifanya badiliko moja kuu ambapo alimwacha mlinda lango Kepa Arrizabalaga nje na kuchezesha Willy Cabalero,hii ni kufuatia tukio lillilotokea siku ya jumapili ambapo Kepa alikataa kufanyiwa mabadiliko kwenye mechi dhidi ya Manchester City baada ya kupata majeraha. Kitendo hicho kilionyesha kukosa heshima kwa mkufunzi na hata kusababisha kushindwa kwenye matuta za penalti na timu ya Manchester city.  Sarri aliamua kumwadhibu kwa kutomchezesha.Aidha mkufunzi huyo amesema kuwa hataki kumwaribia mchezaji huyo kazi kwa hivyo atamchezesha kwa mechi zijazo.Kepa vilevile ametozwa faini ya kutolipwa wiki moja . Chelsea walionyesha mchezo mzuri waliposhinda vijana wa Totenham kwa mabao mawili kwa sufuri .Pedro Rodriguez ndiye aliyetangulia kufanga kabla ya Kieran Tri...

Mahakamani

Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeahirisha kesi inayomkabili Collince Otieno Ogello anayetuhumiwa kupokea pesa kwa njia za udanganyifu. Mbele ya hakimu Joseline Mutehi, mahakama iliambiwa kua mwanamme huyo alipokea pesa kutoka kwa Benard Oyalla, akidai kua yeye ni ajenti wa Eldama comfort house iliyoko mtaani Bandani jijini Kisumu. Benard amesema kuwa alimpa Collince shilingi 10,000 akiahidi kuwapa huduma za Eldama comfort house. Collince Otieno alikanusha mashtaka hayo, na kuomba kuachiliwa dhamana. Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 5 pesa taslimu. Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 9 mwezi April, mwaka huu.

spoti

Image
Timu ya Gor mahia Almaarufu kama Kogalo leo hii itamenyana na timu ya Tusker fc mnamo saa kumi alasiri ugani Kasarani. Kogalo wapo kwenye nafasi ya tatu na pointi 26 kwenye jedwali ya ligi kuu ya kenya KPL baada ya kucheza mechi 13 uko wapinzani wao Tusker wakishikilia nafasi ya sita na pointi 22. Tukisalia mchezoni,mechi mbalimbali za EPL zitarejea leo usiku ili kuendeleza kampeni za kushinda kombe hilo, Mechi hizo zitaanza mida ya saa nne kaso robo ambapo, Arsenal almaarufu kama the gunners watawalika vijana wa Bournemouth ugani emirates. Southampton wataiandaa Fulham fc ugani s.t Marys kabla ya mabingwa watetezi Manchester City kujibwaga ugani Etihad dhidi ya westham united mida ya saa tano kamili. Chelsea watacheza kwao Stamford Bridge dhidi Totenham Hotspurs uko Liverpool wakiandaa Watford ugani Anfield. Manchester Unted almaarufu kama mashetani nyekundu watecheza ugenini Selhust Park dhidi ya Crystal Palace.
Mwanamme mmoja kwa jina Baraka Churchil Otieno , ameshtakiwa kwenye mahakama ya Winam jijini Kisumu kwa kumnajisi msichana mwenye umri wa miaka 11. Mbele ya hakimu Benard Kasavuli, mahakama iliambiwa kua mshtakiwa alitekeleza uhalifu huo tarehe 19 mwezi huu, mtaani Obwola  jijini kisumu. Mshtakiwa alikanusha mashtaka, na kuomba kuachiliwa dhamana. Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 100 pesa taslimu, au shilingi alfu 200 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho. Kesi hiyo itasikilizwa tarehe  11 mwezi Machi, mwaka huu.

Kogalo watishwa

Image
Kocha ya timu ya Hussein Dey kutoka Algeria ametisha kuonyesha Gor mahia madharau walionyeshwa Nairobi kabla ya mechi yao siku ya juma pili waliopoteza kwa mabao mawili kwa sufuri.  Kocha huyo anadai kuwa hawakupewa basi na hata walifanya mazoezi kwenye uga ya kucheza kriketi kisha wakatupiwa vitu kwa uwanja walipokuwa wakichuana.   Kocha huyo ameahidi wanakogalo kuwa pia wao watafanyiwa vivyo hivyo wanapoenda ugenini kule Algeria wikendi.  Amepeleka malalamishi kwa tume ya kusimamia mpira Africa CAF na pia wasimamizi wa mechi hiyo. Kogalo nao wamesema hawaogopi chochote wanapojiandaa kumenyaana siku ya juma mosi kule Algerias na liwe liwalo.  

mwanaume ashtakiwa mahakamani na kosa la kunajisi msichana

Mwanaume mmoja anayefahamika kama Erick Odhiambo amefikishwa mbele ya mahakama ya Winam jijini Kisumu .Erick anatuhumiwa kumnajisi msichana mwenye umri wa miaka kumi na saba. Mbele ya hakimu Fatuma Mwanza Rashid, mahakama iliambiwa kua bwana Erick alifanya kitendo hicho mnamo tarehe 20 mwezi huu wa February kwenye mtaa wa mamboleo iliyoko kisumu. Erick alikanusha mashtaka hayo, na kuomba kuachiliwa dhamana. Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 125 pesa taslimu, au shilingi alfu 250 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho. Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 9 mwezi Mei, mwaka huu.

Haki za Mashoga na Wasagaji

Image
Mahakama kuu ya Mlimani iliyoko jijini Nairobi iliairisha kesi inayohusisha wakenya wenye uhusiano za kimapenzi na jinsia moja hadi takriban mwezi mbili zijazo. Kesi hiyo linalenga kupea mashoga haki kwenye katiba na kuhakikisha kwamba serikali limekubali ndoa ya watu wenye jinsia moja. Mashoga hao wanataka haki zao ziheshimiwa na waache kudharauliwa na hata kupuuzwa mtaani kwa kuwa sio hatia kuchagua kupenda mwanamke ama mwanume mwenzako. Kumbuka ushoga ni hatia kubwa sana kwenye katiba ya kenya na mtu anayepatikana kujihusisha na mpenzi ya jinsia moja anafaa kufungwa jela miaka kumi na nne kulingana na kifungo 162(a) na 162(c) ya katiba ya Kenya. Nilipozungumza na wakazi wa kisumu,baadhi yao walikana sana mapenzi ya jinsia moja na kusema kwamba ni jambo linalokanwa hata kwa bibilia. Ilhali kuna wale ambao walikubaliana na mapenzi ya jinsia moja na kusema wanamatumaini kwamba watu wenye jinsia moja watapata haki na kuweza kuishi na kupenda bila uoga uku nchini Kenya. Je Mas...

Mlinda Lango Wa Chelsea,Kepa Alaumiwa Kufuatia Kichapo Cha Man City

Image
https://www.goal.com/en-ke/news/shameful-kepa-blows-it-for-unlucky-chelsea-with-sarri-mutiny/dhuz9p3pnmg91j5chkhelqkd0 Timu ya Chelsea ilionyesha mchezo mzuri kwenye fainali za kombe la carabao dhidi ya Manchester City iliochezwa jumapili usiku kabla ya mlinda langu wao Arrizabalaga Kepa kudinda kubadilishwa  Timu zote zilikuwa sare ya kutokuwa na bao na ilikuwa dhahiri shairi kuwa mshindi angejulikana kwa matuta za penalti. Mlinda langu wa akiba Willy Cabalero alikuwa tayari kuingia baada ya Kepa kupata majeraha lakini mlinda langu huyo akasema ako sawa na kunyima Cabelero 'ambaye ana ujuzi sana kwa kushika matuta za penalti nafasi ya kuokoa ''The Blues'. Kitendo hicho kilikasirisha sana Maurio Sarri ambaye ako kwa hali mbaya sana na uhenda akapoteza kazi yake.Sarri alisema kwamba atazungumza na Kepa ili kujua shida kubwa linaeza kuwa wapi. Mchezaji Eden Hazard na Ngolo Kante walionyesha mchezo mzuri na hivyo kupatia mashabiki matumaini kuwa chelsea wangeshind...

Eufa Europa League

Mechi za Eufa Europa League zilirejea usiku wa Alhamisi kwa raundi ya 32 ambapo mechi mbalimbali zilichezwa kwenye uga tofauti. Arsenal walilaza vijana wa Bate kwa mabao tatu kwa sufuri ugani emirates,Redbull ikashinda timu ya club Brugge kwa mabao manne kwa sufuri,Eintrach ilishinda Shahktar Donestk kwa mabao manne kwa moja,Villareal wakatoka sare ya moja kwa moja dhidi ya Sporting,Dinamo Zagreb walishinda Plzen kwa mabao tatu kwa sufuri,uko Zenit wakilaza Fernabache kwa mabao tatu kwa moja,Valencia waliponyoka na bao moja dhidi ya Celtic,uko Napoli wakashindi mbili kwa sufuri dhidi ya Fc Zurich,Timu ya Genk walishindwa na Slavia Praha kwa mabao manne kwa moja uko Inter milan ikilaza Rapid Wien kwa mabao manne kwa sufuri. Vilevile Bayern Liverkusen walilazimishwa kutoka sare na Fc Krasnodor,Benfika pia nao wakatoka sare bila bao dhidi ya Galatasary,Real Betis walishindwa kwao na Rennes kwa mabao tatu kwa moja,Dynamo Kyiv walishinda kwa bao moja kwa sufuri dhid...

RAW LAW⁉⁉

 RAW LAW⁉⁉  If laws could speak for themselves🗣 They could complain of lawyers 👨🏼‍⚖in the first place Law practice has become the complete opposite of sex🙀 When it is good it has to come through deluxe🤬 With corruption Manning the world😖 Without money you are untold🤢 Criminals know their rights🕵 By which they claim to fight📚 All systems hacked🎛 Honest ones expensively backed📲 We no longer know what is wrong or right🤐 For a say is contained in the might💪 It is said that a good lawyer knows how the law to punch👊 While the clever one takes the judge for lunch🍝 And being clever🤒 Is all we endeavour🤖 So is gonna be raw🤯 Or are we handling law📖🔖

zilizotokea mahakamani

Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeahirisha kesi inayomkabili Fredrick Odhiambo anayetuhumiwa kwa kesi mbili kujifanya polisi na pia kumiliki madawa za kulevya.  Mbele ya hakimu Benard Kasavuli, mahakama iliambiwa kua bwana Ezekiel alipatikana mnamo tarehe ishirini mwezi huu maeneo ya kondele iliyoko kisumu akiwa na bhangi 'roals' tatu  na uko akijifanya kuwa polisi. Fredrick alikanusha mashtaka hayo, na kuomba kuachiliwa dhamana. Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 50 pesa taslimu, au shilingi alfu 10 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho. Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 6 mwezi ujao mwaka huu.
Timu ya Atletico Madrid ilicharaza vijana wa Juventus kwa mabao mawili kwa sufuri kwenye mkondo wa kwanza za mechi za raundi ya kumi na sita ya kombe la Eufa.Mechi hiyo ilichezwa usiku wa jumanne kwenye uwanja wa Wanda Metropolitano nyumbani kwa Atletico madrid. Atletico walipata bao lao la kwanza kupitia kwa defender wao Jose Gimenez mnamo dakika ya 78 kabla ya Diego Godin kuongeza la pili dakika tano baadaye. Juhudi zake mchezaji bingwa Christiano Ronaldo kupatia timu yake ushindi iligonga mwamba na hata za mwenzake mpotugali Diblo Dyballa pia hayakufua dafu uko wakishindwa na Vijana wa Diego Simeon. Kwingineko,Vijana wa Pep Guardiola Manchester City walishinda Schalke 04 kwa mabao matatu kwa mawili ugenini  Veltins Arena kwa wanaSchalke04. Manchester city ndiye waliotangulia kufunga mnamo dakika ya 18 kupitia kwa mchezaji Sergio Kun Aguero lakini wanaSchalke 04 walijibu kwa mpigo kwa mabao mawili mnamo dakika ya 38 na 45 mtawaliwa,bao zote za schalke zilifu...

mchezoni

Ligi kuu nchini KPL itarejea leo kwa mechi moja ambapo Gor Mahia almaarufu kama Kogalo wataandaa vijana wa western stima kwenye uga wa Moi International Sports Centre,Kasarani.Mechi hiyo itachezwa saa kumi alasiri.Kumbuka Kogalo wako nafasi ya tatu kwenye jedwali ya ligi wakiwa na alama 25 baada ya kucheza mechi 12{mechi moja nyuma ya viongozi Bandari ambao wako na alama 28},Western Stima nao wako nafasi ya 7 na alama 20. Kwingineko mechi za kombe la Eufa ziliendelea usiku wa juma nne kwa mechi mbili tofauti.Barcelona walilazimishwa kutoka sare bila bao lolote ugenini kwa Olympique Lyonnais,juhudi zake mchezaji bingwa Lionel Messi kupatia timu yake bao iligonga mwamba na kuwalazimisha kugawa alama. Liverpool pia walitesa nyasi bure ugani Anfield walipoandaa Bayern Munchen. Mechi zingine zitaendelea leo usiku ambapo Atletico Madrid wataandaa Juventus,vilevile Fc Schalke 04 watakaribisha vijana wa Manchester city.Mechi zote zitachezwa kuanzia saa tano.

Nature is my best friend🤞

Nature is my best friend🤞 Cause with it I have nothing to mend🌚 Each morning am awake😌😌 Am glad to see the earth's orange cake☀ Spreading out its rays with glee🌞 You don't have to be on your knee🛐 To get its warmness🌤 It gives a reason for gladness😊😊 That no matter how dark is the night🌑 Mornings will ever be bright☀☀ The dew on the ground❄ Bring a meaning in the heart to be wound💝 Things may happen in your life😏 Which may cut across like a sharp knife🤺 But when you allow light to shine on you💫 All these obstacles will forsake you and you become new✨ The nine o'clock sun Will give you strength💪 As it makes our bones active and prevents us from stench🤧 This comes when the day is still young😇 To mean we got all it takes when still young🧖‍♂ Don't waste your youthful life not a tone🤒 For there is no life rehearsal none🙅🙅 The sun becomes scorching hot at noon🔥🔥 You may think the world is ending soon🤯 At a point in life things may seem high😯 But don...

kesi mahakamani

 Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeahirisha kesi inayomkabili Ezekiel Nyambane anayetuhumiwa kufanya biashara bila leseni . Mbele ya hakimu Benard Kasavuli, mahakama iliambiwa kua bwana Ezekiel alipatikana mnamo tarehe kumi na nane mwezi huu akiuza madawa kwenye duka la dawa moja liitwalo kama Ziwa iliyoko kisumu. Ezekiel alikanusha mashtaka hayo, na kuomba kuachiliwa dhamana. Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 10 pesa taslimu, au shilingi alfu 20 na mdhamini wa kiasi sawa na hicho. Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 18 mwezi Juni, mwaka huu.

Sarri taabani

 Timu ya Chelsea hawakutuzwa kwao Stamford Bridge walipolazwa mabao mawili kwa sufuri na timu ya Manchester United kwenye mechi ya raundi ya tano ya kipute cha FA jana usiku.Hivyo basi chelsea  wamebanduliwa kutoka kwa mashindano hayo. Matokeo hayo yanauweka uongozi wa mkufunzi wa Chelsea Sarri katika hali mbaya,huko united ikijibu baada ya kushindwa kwa mara ya kwanza chini ya ukufunzi wa Ole Gunna Soljkskjear na kujinyakulia nafasi kwenye robo fainali dhidi ya Wolvehampton. Ander Herrera alifunga bao la kwanza baada ya kupata krosi nzuri kutoka kwa Paul Pogba mnamo dakika ya 31 kabla ya Pogba kuongeza bao la pili kupitia kichwa dakika chache kabla ya mapumzikoni. Tukisalia mchezoni,Liverpool itaiandaa Bayern Munchen kwenye mechi ya kikundi cha Eufa leo usiku. Mechi hiyo itachezwa ugani Anfield kuanzia saa tano za usiku. Vilevile Timu ya Barceleona itakuwa ugenini dhidi ya Olympique Lyonnais kwenye kampenzi za kombe hilo la Eufa,

Mahakamani:wanawake taabani

 Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeahirisha kesi inayomkabili Fiona Awino anayetuhumiwa kuumwibia mwajiri wake kwa jina la purity Anyango . Mbele ya hakimu Fatuma Mwanza Rashid, mahakama iliambiwa kua mwanadada huyo alimwibia mdozi wake pesa takriban elfu hamsini na nane na mia sita mnamo juma mosi tarehe kumi na sita mwakani uko mtaa wa car wash iliyoko kisumu. Fiona alikanusha mashtaka hayo, na kuomba kuachiliwa dhamana. Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 50 pesa taslimu, au shilingi laki moja na mdhamini wa kiasi sawa na hicho. Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 8 mwezi Aprili, mwaka huu. Tukisalia mahakamani,Samantha Atieno alikubali mashtaka baada ya kuhutumiwa kuuza pombe bila leseni kwenye mtaa wa molem ilioko jijini kisumu.Alitozwa faini ya alfu ishirini ama mwezi sita gerezani.

LIGI KUU NCHINI,KPL

Mechi za  KPL ziliendelea jana kwenye uga tofauti nchini.  Mechi izo ziling'oa nanga mnamo saa nane mchana na mchuano kati ya KCB Fc na Vijana wa Sony sugar  kwenye uga wa Kenyatta stadium Machakos ambapo vijana wa KCB walishinda kwa bao moja kwa sufuri.Mechi zingine zilikuwa  pamoja na ya Zoo Kericho wakichuana na mathare united kwenye uga wa green stadium Kericho mechi iliyoisha sare ya kutokuwa na bao lolote. kwingineko posta rangers walishinda vihiga united kwa bao moja kwa sufuri kule mumias sports complex ilioko mumias.Western stima nao pia walichapa vijana wa mount kenya kwa mabao mawili kwa moja kule moi stadium kisumu. Vilevile Ulinzi stars walicharaza AFC Leopards kwa bao moja kwa sufuri mechi iliyochezwa kule Kenyatta stadium machakos. Shughuli hayo hayakuisha kabla ya vijana wa Gor mahia almaarufu kama Kogalo kulaza sofapaka kwa bao moja kwa sufuri kwenye mechi ya kukata  na shoka iliyochezwa kwenye uga wa Moi International sports centre N...

Mchuano za KPL

Mechi za kung'ang'ania kombe la KPL zitaendelea wikendi hii kwenye uga tofauti nchini.Kumbuka Mathare united ndiye bado wanaongoza kwenye jedwali ya kombe hilo.  Mechi izo zitang'oa nanga kesho mnamo saa nane mchana na mchuano kati ya Mount Kenya United Fc na Viongozi wa jedwali Mathare united kwenye uga wa Nyayo jijini nairobi.Kisha posta rangers watajibwaga ugani kipchoge keino stadium kuchuana na Tusker fc mnamo saa tisa jioni.Vilevile Ulinzi stars watacheza na  chemelil ugan Afraha iliyoko nakuru mnamo saa kumi na robo. Mech zingine zote zitaendelea siku ya jumapili saa tisa jioni zikiwemo Kakamega homeboyz dhidi ya Vihiga united kwenye uga wa Afrah.Nzoia sugar pia watacheza dhidi ya Sony Sugar kwenye uga wa Masinde Muliro iliyoko Bungoma . Vilevile Mabingwa wa kombe la sportpesa kariobangi Sharks pia wataendeleza kampeni  zao dhidi ya sofapaka fc ugani Nairobi city stadium.Vijana wa Zoo kericho pia watamenyana na Kenya Commercial Bank ugani Green...

Waaguzi watisha kugoma

Kuna hofu baina ya wakazi wa kisumu hasa jamaa na marafiki za wagonjwa katika mahospitali mbalimbali za uma.Hii wasiwasi inakuja baada ya shirikisho linalosimamia waaguzi kuonya kuwa wataenda mgomo mnamo Juma tatu tarehe nne mwezi huu.Waaguzi hao wanadai kuwa serikali haijatimiza makubaliano yao ya kuwapa marupurupu mbalimbali na kupandishwa cheo kutokana na maelewano kati yao mnamo November 2011. Tulipozungumza na mkurugenzi mkuu wa Afya wa Kisumu county bwana Stephene Otieno Sewe alisema bado wanafanya juhudi zote kuhakikisha kwamba matakwa ya waaguzi hao yametatuliwa. Tukisalia kwa habari za afya,wakazi wa kisumu bado wanajitokeza kwa sehemu tofauti ya kaunti ili kusajiliwa na uhc.Kumbuka shughuli hiyo ya kusajili watu ilifaa kukamilisha jana tarehe 31 lakini imesukumwa mbele hadi tarehe 23 mwezi huu ili kupatia muda wale ambao hawajajisajili kuja kujiandikisha . Mkurugenzi mkuu wa afya,kisumu kaunti Bwana Stephene Otieno Sewe ameimiza wakazi wa kisumu kujitok...