Timu ya Kakamega Homeboyz wameshinda vijana wa Bandari Fc kwa mabao manne kwa sufuri ugani Bukhungu stadium kakamega.Mchezaji Alan Wanga alicheka na wavu mara mbili alipofunga bao la kwanza na la tatu mnamo dakika ya 26 na 65 mtawalia.Peter Thiong'o pia alijiheka kwenye kitabu cha wafunga bao alipoheka bao la pili mnamo dakika ya hamsini na saba uku Moses Mudavadi akikamilisha shughuli izo alipofunga bao la mwisho dakika ya themanini na moja.
vilevile Timu ya Zoo Kericho walifungiwa bao la kipekee kupitia  mchezaji Kevin Omondi dhidi ya Fc Leopards ugani Green stadium ,Kericho.
Kwingineko mabingwawa kombe la sportpesa Kariobangi sharks walitesa nyasi bure walipotoka sara ya suluhu bin suluhu dhidi ya viongozi kwenye ligi,Mathare united.Mechi iliyochezwa Nairobi City stadium.
Tukisalia mchezoni,mabingwa mara kumi na saba kwenye kombe za KPL Gor mahia wameshinda wapinzani wao wakali Sony sugar mabao mawili kwa sufuri.Bao zote zilifungwa na Jaqcuis Tuyisenge mnamo dakika ya 30 na 60 ugani Green stadium Awendo.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals