kesi mahakama

Mahakama ya Winam jijini Kisumu, imeahirisha kesi inayomkabili Nancy Awuor anayetuhumiwa kupokea pesa kwa njia za udanganyifu.
Mbele ya hakimu Bernard Kasavuli, mahakama iliambiwa kua mwanadada huyo alipokea pesa kutoka kwa Dorcas Atieno na Damaris Atieno, akidai kua angewauzia bidhaa mbali mbali.
Dorcas amesema kuwa alimpa Nancy shilingi 55,000 akiahidi kumuuzia jokovu au friji na runinga.
Damaris naye amesema kua alimpa Nancy shilingi 25, 000 akiahidi kumuuzia home theatre, mnamo tarehe tisa mwezi wa Sita mwaka jana.
Nancy Awuor alikanusha mashtaka hayo, na kuomba kuachiliwa dhamana.
Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi alfu 70 pesa taslimu, au shilingi laki mbili na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 14 mwezi Mei, mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals