Foleni kwenye usajili ya UHC

Wakazi wa Kisumu leo hii walijaa kwenye foleni ya kujiandikiza na UHC kwenye sehemu tofauti jijini,wanamatumai kuwa watapokea matibabu za bure iwapo wataugua hapo mbeleni.UHC ni mojawapo kati ya ajenda nne kubwa za serikali mwaka huu na kaunti ya kisumu ni moja wapo kati ya zile kaunti nne zikiwemo Isiolo,Machakos na Nyeri zilizochaguliwa.
Nilipozungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza kwa shughuli izo kwenye uga ya kucheza ya JomoKenyatta,wamesema kuwa wanatumai UHC itasaidia wananchi wengi sana hasa wasio na uwezo wakujilipia matibabu.
Vilevile Cathy Oduol ambaye ni ajenti ya UHC jijini kisumu pia ameongeza kuwa mkenya yeyote anaweza jiandikisha na UHC bora awe na kitambulisho na pia watoto wenye umri kati ya mwaka moja hadi ishirini na tatu wanaweza jiandikisha pia.
wale amabao wamejisajili tayari lakini bado wangependa kuongeza watu kwenye kadi yao wanaimizwa kufanya hicyo kabla ya tarehe thelathini na moja mwezi huu ambapo shughuli hizo zitaisha.

Comments

Popular posts from this blog

Mahakamani

Jeshy Tisa Ya Kogalo wabandua Petro Atletico!

Brazil Sent Packing As Croatia Proceeds To Semi Finals